Thursday, June 28, 2012

LIONS CLUB YACHIMBISHA VISIMA SHULE ZA MSINGI MINAZI MIREFU NA AIRWING KIPAWA JIJINI DAR

Diwani wa Kata ya Kipawa Bonah Kaluwa, akifungua moja ya bomba la maji ya kisima walichokabidhiwa na wahisani hao katika Shule ya Msingi ya Airwing Kipawa. Diwani Kaluwa ndiye aliyefanikisha mpango wa upatikanaji wa visima hivyo kupitia Lions Club.
Gavana wa Lions Club Internation Tanzania na Uganda, Satish Sherma, akitoa hotuba fupi kabla ya kukabidhi visima hivyo.
Gavana wa Lions Club Internation Tanzania na Uganda, Satish Sherma, akimvalisha beji ya Lions Club, Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa wakati wa makabidhiano ya visima hivyo.
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa (wa pili kulia), akizungumza jambo na Gavana wa Lions Club Internation Tanzania na Uganda, Satish Sherma (kushoto) na Katibu Mkuu wa Lions Club, Mustafa Kundrat.
Wanafunzi wa Shule za Minazi Mirefu na Airwing wakipiga makofi wakati wa kukabidhiwa visima hivyo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya Msingi Minazi Mirefu, Daniel Mwamakula (kulia), akitoa neno la shukurani kwa wahisani hao na wageni waalikwa.
Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kulia), akimkabidhi fedha Bakari Ally ambaye alikuwa msimamizi wa ujenzi wa visima hivyo.

No comments: