Thursday, June 28, 2012

YANGA SPORTS YAFANYA MAZOEZI KUJIFUA KAGAME CUP

Kifaa kipya cha Yanga, kutoka Simba Kelvi Yondani, akipiga mpira wakati wa mazoezi ya timu hiyo kujifua kwa ajili ya kujiweka sawa na mashindano ya Kombe la Kagame, mashindano yatakayofanyika jijini Dar es Salaam.
Mshambuliaji mpya wa Yanga, Simon Msuva (mbele), akiwaongoza wenzake katika mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika kwenye fukwe za Coco Beach jijini Dar es Salaam jana. Wanaomfuatia ni beki mpya wa klabu hiyo, Kelvin Yondani na Godfrey Taita. (Picha zote na Mpiga Picha wa Habari Mseto Blog).
Nurdin Bakari akijifua wakati wa mazoezi hayo jana.
Nizar Khalfan (kushoto), akijifua na wachezaji wenzake wa Yanga katika mazoezi hayo.
Mmoja wa wachezaji wapya wa Yanga akiwa kwenye mazoezi hayo.

Wachezaji wa Yanga wakikimbia katika mazoezi mepesi ya kujiandaa na mashindano ya Kagame Cup yanayotarajiwa kuanza Julai 14 jijini Dar es Salaam.
Nizar Khalfan akiwa katika mazoezi na timu yake mpya ya Yanga katika ufukwe wa Coco Beach Oysterbay jijini Dar es salaam.
Wachezaji wa Yanga wakipiga danadana, wakati wa mazoezi yao kwenye ufukwe wa Coco Beach, jijini Dar es Salaam leo.

No comments: