Thursday, June 28, 2012

MBUNGE ZUNGU (ILALA) AKUTANA NA WAKAZI WA SHARIF SHAMBA JIJINI DAR

Mkazi wa Sharifu Shamba, Abdallah Kondo, akitoa duku duku lake kwa Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan 'Zungu', wakati Mbunge huyo, alipofika eneo hilo kwa ajili ya kusikiliza matatizo ya wapiga kura wake na kuzungumza nao jijini leo. (Picha zote na Kassim Mbarouk)
Baadhi ya wakazi wa Sharif Shamba, wakisikiliza hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na baadhi yao kuhusu matatizo yanayowakabili kwenye eneo lao hilo, mbele ya Mbunge wao, Mussa Zungu, wakati alipowatembelea kusikiliza matatizo yao leo.
Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan 'Zungu', (wa pili kushoto), akiwa na Diwani wa Kata ya Ilala, Edson Fungo (wa tatu) na Mwenyekiti wa mtaa wa Sharif Shamba, Mtoro Shah, wakisikiliza hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na wakazi wa mtaa huo, wakati alipofika eneo hilo kwa ajili ya kusikiliza matatizo ya wapiga kura wake na kuzungumza nao jijini leo.
Mkazi wa Sharif Shamba, Ilala jijini Dar es Salaam, Mariam Mkupama, akitoa baadhi ya kero zinzowakabili mtaani hapo kwa Mbunge wao Mussa Zungu, alipokuwa akisikiliza matatizo yao yanayowakabili mtaani hapo leo.
Baadhi ya wakazi hao wakiwa katika mkutano huo leo, wakisikiliza masuala mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa na baadhi yao kwa Mbunge wao Mussa Azzan Zungu, alipofika mtaani hapo kusikiliza matatizo yao na kuzungumza nao.
Mbunge wa Ilala, Mussa Zungu (wa pili kushoto), akiwa na uongozi wa Kata ya Ilala na wa mtaa wa Sharif Shamba, akinakili matatizo na hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na kuwasilishwa kwake na wakazi wa Sharif Shamba, wakati alipokwenda kusikiliza matatizo yao pamoja na kuzungumza nao leo jioni.
Bi. Mtumwa Abdallah, akitoa matatizo yanayowakabili mtaani hapo mbele ya Mbune wa Ilala, Mussa Zungu (hayupo pichani), aliyotaja kuwa ni adha ya magari makubwa ambayo huuingizwa mtaani hapo na kusababisha kukata waya za umeme, hatua inayopelekea kuikosa nishati hiyo mara kwa mara.
Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan 'Zungu', (wa pili kushoto), akisoma moja ya barua aliyokabidhiwa na mmoja wa wakazi wa mtaa wa Sharif Shamba, kuhusiana na njia mbalimbali alizokuwa akipitia katika kutatua baadhi ya matatizo yao lakini bila kupata mafaniko yoyote yale. Wa tatu ni Diwani wa Kata ya Ilala, Edson Fungo, Mwenyekiti wa mtaa wa Sharif Shamba, Mtoro Shah (wa kwanza kushoto) na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa mtaa huo, Zadock Munisi, wakiwa katika mkutano huo.
Baadhi ya akinamama wakazi wa mtaa wa Sharif Shamba, wakisikiliza hoja mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa kwa Mbunge Zungu leo jioni.
Wananchi wakazi wa mtaa huo, wakimsikiliza Mbunge wao, Mussa Zungu alipokuwa akijibu hoja zao, walizokuwa wakizitoa kwake na kwa uongozi wa Kata na mtaa wao huo.
Mbunge wa Ilala, Mussa Zungu akizungumza na wakazi wa mtaa wa Sharif Shamba mara baada ya kusikiliza hoja na matatizo yao kwenye mkutano wao huo leo jioni.
Baadhi ya wakazi wa mtaa huo, wakimsikiliza Mbunge wao, Mussa Zungu, wakati alipokuwa akizungumza nao kwyenye mkutano huo leo jioni.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Sharif Shamba, Mtoro Shah, akijibu baadhi ya tuhuma alizokuwa ametuhumiwa na kuwasilishwa kwa mbunge Zungu (kulia), kwenye mkutao huo.
Mbunge wa Ilala, Mussa Zungu (katikati), Diwani wa Kata ya Ilala, Edson Fungo (kulia) na Mwenyekiti wa mtaa wa Sharif Shamba, Mtoro Shah (kushoto), wakisikiliza maelezo mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa kwa awamu ya pili na wakazi wa Sharif Shamba kwenye mkutano huo leo jioni.
Mkazi wa mtaa huo, Sakina Juma, akiwasilisha kwa Mbunge Zungu kilio chao, mtaani hapo, ikiwemo tatizo la maji na kuaharibika kwa pumpu ya kisima chao kirefu cha maji wanayotumia mtaani hapo, ambapo katika jibu lake Mbunge Zungu aliahidi kushughulikia tatizo hilo haraka ikiwemo kutoa tenki la kuhifadhia maji ya matumizi ya mtaa huo.
Mbunge Mussa Azzan Zungu, akizungumza na wakazi hao wakati alipokuwa akihitimisha mkutano wake na wakazi hao katika kusikiliza matatizo yanayowakabili pamoja na kero mbalimbali mtaani hapo. Wa pili kulia ni Diwani wa Kata ya Ilala, Edson Fungo, Mwnyekiti wa mtaa huo, Mtoro Shah (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM wa tawi la Sharif Shamba, Zadock Munisi

No comments: