Thursday, June 28, 2012

PICHA: MATUKIO BUNGENI


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (kushoto) na Mbunge wa Viti Maalum, Leticia Nyerere kwenye viwanja vya Bunge, Mjini Dodoma leo Juni 27,2012.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Mbinga Mashariki Gaudence Kayombo, kwenye jengo la utawala la Bunge Mjini Dodoma leo Juni 27,2012.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimina na Mbunge wa Dole, Sylvester Mabumba, viwanja vya Bunge Mjini Dodoma leo Juni 27, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wawekezaji katika sekta ya madini mkoani Mara kutoka kampuni ya Gemini Corporation ya Urusi, ofisini kwake Bungeni mjini Dodoma leo Juni 27,2012. Kushoto ni mwenyeji wao , Mbunge wa Viti Maalum Zainab Kawawa.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na akinamama wawekezaji katika sekta ya madini, mkoani Mara kutoka Kampuni ya Gemini Corporation ya Urusi mara baada ya mazungumzo yao leo.


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na wawekezaji katika sekta ya madini mkoani Mara kutoka kampuni ya Gemini Corporation ya Urusi baada ya kuzungumza nao, Ofisini kwake Bungeni Mjini Dodoma leo Juni 27,2012. Kushoto ni Mwenyeji wao , Mbunge wa Viti Maalum Zainab Kawawa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri wa Fedha, William Mgimwa, akibadilishana mawazo na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, nje ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo.


Mbunge wa Jimbo la Nkenge, Assumpter Mshamba (CCM), akichangia bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, bungeni mjini Dodoma leo.


Mbunge wa Moshi mjini, Phillemon Ndesamburo (Chadema), akisalimiana na mjasiriamali, Emma Kawawa, ambaye ni mtoto wa mwanasiasa mkongwe amabye sasa ni marehemu Rashid Mfaume Kawawa, walipokutana kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma leo. Kulia ni Mbinge wa Viti Maalum, Lucy Owenye (Chadema), ambaye ni mtoto wa Ndesamburo.


Waziri Mwakyembe akichangia bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu bungeni mjini Dodoma leo.

Mbunge wa Viti Maalum kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Lucy Kiwelu, akichangia bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu bungeni mjini Dodoma leo.
Waziri wa TAMISEMI, Hawa Ghasia, akizungumza jambo na Mwenyekiti wa CHADEMA, ambaye ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzania Bungeni, Freeman Mbowe, nje ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma.

No comments: