Wednesday, August 22, 2012

JUMUIYA YA WATANZANIA DC (DMV) KUFANYA PICNIC NA PARTY LA NGUVU 8/25/2012

Tanzania Community DMV with the Free good Food BBQ and more@ Regional Park 2000 Shorefield Road @ Wheaton, MD

And Same night is going down with the Full Disco Fiesta. NJOO ULISAGE RUMBA@ 4911 Prince Goerges Ave, Belsville MD 20705

From 9:PM UP2 2:AM, Kujaa Kulisakata Rumba
Get Your Summer Party with the Tanzania Community in DMV Full Disco Fiesta Patrieeeee is going on.!!








BREAKING NEWSSSS!!! MSANII DIAMOND KUELEKEA MAREKANI

Msanii wa Bongo Flavor Diamond kuelekea Marekani kwa kozi maalum.Pia kutumbuiza Washington DC. Habari zaidi, zikipatikana. Bongo flava inalipa kumbe.

UZUSHI UNAOSAMBAZWA NA WATU KUHUSU JUMUIYA YA UONGOZI WA WATANZANIA DMV

KUMEKUWA NA UZUSHI UNAOSAMBAZWA NA WATU WACHACHE ILI KUIBOMOA JUMUIYA YA WATANZANIA WASHINGTON DC, MARYLAND NA VIRGINIA. WATU HAO WANADAI KWAMBA UONGOZI UMEPOKEA RUSHWA KUTOKA CHAMA KIMOJA CHA SIASA CHENYE TAWI LAKE PALE DMV, WATU HAO PIA WAMESHINDWA KUJITAMBULISHA NA KUAMUA KUTUMIA MAJINA BANDIA KITU AMBACHO KINAWAFANYA WENGI WAAMINI WATU HAO HAWANA UHAKIKA AU HAWAJUI WANACHOONGEA. 

Tunataka kuwarahisishia watu hawa na madai yao, wanachotakiwa kufanya ni;

(a) Wajitambulishe ni akina nani.
(b) Waje na ushahidi wa madai yao.
(c) Ni sheria ipi ya katiba ya Jumuiya iliyovunjwa
AU WAKISHINDWA KUTHIBITISHA MADAI YAO
(d) Basi wakae kimya cuz they are full of sh*t, na waache jumuiy ifanye kazi na wapunguze chuki n porojo. Tuhuma hizi nig maneno tu hata kwenye kanga yapo.

NB. Toleo hili halijatolewa na uongozi wa Jumuiya na wala halihusiani na yoyote ndani ya uongozi.
NB. Blog hii haihusiki na ujumbe hapo juu.

Friday, August 17, 2012

WATANZANIA WA CHAMA KIMOJA CHA SIASA WASHINGTON DC WAANZISHA VITA YA MATUSI DHIDI YA CCM NA WATANZANIA WENZAO



KUNA UKURASA WA FACEBOOK PAGE ULIOFUNGULIWA NA WATANZANIA WANAOISHI HAPA DMV NA KUTUKANANA MATUSI MATUSI YA NGUONI NDANI YA MWEZI MTUKUFU HUU WA RAMADHANI.

Kuna page inaitwa XXXXXXXXXXXXXXX


Page hii inasemekana imefunguliwa na waTanzania wanaoishi hapa hapa Maryland wengine ni wavulana ambao wanajiita majina ya kike kutukana waTanzania wenye idikadi tafauti kwakuwa tu wanachuki binafsi na kuleta uhasama katika Jumuiya yetu, na wengine ni wasichana ambao nafsi zao zinavutwa na uhasama na chuki, pamoja nakujiingiza katika kundi ambalo hawastahili kuwemo alimradi tu wanafuata mkumbo na kusahau kuangalia malengo ya maisha yao kwa ujumla.

Chakushangaza wanajiita majina ya kiislamu na kutukana Matusi yanguoni ndani ya mwenzi huu wa Mtukufu wa Ramadhani, watu hao nina uhakika katika urafiki wa Facebook page zetu, tunao, na kule walipo wamejivalisha ngozi za nyoka kwa kubadili majina yao, katika mshuhuli mbali mbali ya kijumuiya pamoja na yakibinafsi, tunakuwa nao, chakushangaza zaidi wanadhani hawajulikani kumbe mitaani tayari wanajulikana juu ya hilo ila watu wanawaangalia mwishowao utafika wapi..?

Kumuweka mtu picha yake na kuanza kumtusi matusi yanguoni.

Hizi ni nafsi chafu ziliyojaa uadui uwovu na majivuno yakiambatana na kiburi na kutafuta kukomoana, pasipo sababu za maana. Hakuna tabia mbaya katika tabia za binadamu na yenye kuchukiwa kama tabia hizi ambazo katika jamii yetu sasa hivi zimetawala hata sijui watu hawa wamekusudia nini katika maisha yao ya baadae.

Kama tabia hizi zikiachiwa na kuendelea katika jumuiya yetu, zitamea kwenye nafsi zetu tutaanza kuondoa mfungamano wa kirafiki wa kindugu na hata majadiliano yetu hukosa busara na hikma kiasi cha kupelekea kwenye utengano na uhasama na chuki miongoni mwetu hapa.

Yote kutokana na utulivu wa nafsi, yanaotokana na tabia mbaya ya hasira ya kushindwa katika mihemko ya kutafuta maisha au kushindwa kwake katika kile unachokitafuta katika kuboresha maisha yake, kiasi ya kuvuruga mtiririko wa fikra chanya na kupelekea kuvuruga uthabiti wa kiroho juu ya mtu. Huenda ni kutokana na sababu Fulani fulani za kukosea hapa na pale au kujaribu hiki na kile, hamaki zake kupelekea kuwachukia wale waliojituliza kimaisha, kiasi ya kwamba kwa wale wasio na utulivu na uvumilivu uamua kuwasingizia mambo haya na yale wale wanao waona kuwa ni maadui zao.

Tabia hizi ni zawatu wachache tu walio katika kundi hili linaloitwa XXXXXXXXXXX limekuwa ni gumzo katika jamii yetu hapa DMV, kujihusisha katika Malimbano yaliokuwa si yalazima.

Nilijaribu kuingia katika kundi hilo na kutoa nasaha zilizobora pamoja na kuwakanya kuacha tabia hiyo mara moja, amaa sheria itafuata mkondo wake, matukeo yake niliambatia matusi na dada mmoja anajiita (Rukia Shabani) Na matokeo yake wakani toa katika kundi hilo, kuna baadhi ya watu ambao wamehusishwa katika kundi hilo wanafuatila kwa makini pamoja na kuwa Record zote tunazo na ushahidi wa baadhi ya watu waliotukanwa pamoja na maoni yao waliyatoa juu ya sakata hilo la matusi ya nguoni.

Tunajua Njia mojawapo ya kuishi kwa amani ni kuwa na utulivu wa moyo na kusahau mabaya ya watu hao huku tukizingatia umuhimu wa maisha yetu kwa kujaribu au kujitahidi kuishi kwa roho safi na huyapuuza mabaya na upinzani wa kiadui tunaokuta .

Hii ndio kazi yetu kutunza kumbukumbu juu ya yale yanayoendelea katika jamii yetu, hatutokaa kimyaa kuona uchafu kama huu unamea katika Jumuiya yetu na kudhalilishwa wengine ilimradi kufurahisha nafsi za watu wachache ambao tunauwezo wa kuwadhibiti.

Naomba mawazo na fikra zako tufanye nini ili tupunguze Uhasama na chuki zilizojaa ndani ya jumuiya yetu...?


chanzo ni mdau wetu wa marekani swahilivilla

Saturday, August 4, 2012

CCM YAFUTURISHA JIJINI WASHINGTON DC (DMV)

Saturday, August 4, 2012

Makada wa CCM wakiwa na kadi za uwanachama kwa wanachama wapya katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akipata picha na tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha CCM, katika futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Tikiti maji lililochongwa kwa longo ya Chama cha Mapenduzi CCM

Baadhi ya waTanzania mbali mbali waliohudhuria kwenye futari hiyo ilioandaliwa na tawi la CCM DMV

Baadhi ya waTanzania waliovalia rangi za chama cha CCM wakiwa kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.

Makada wa CCM Tawi la DMV shoto Mbunifu wa Ma Winny Casey Khanga Wrap Designer, pamoja na Peter Ligate (Picha ya kulia) wakiwa katika mpango mzima wa futari ya pamoja ilioandaliwa na wanatawi la CCM DMV

Watanzania waliojumuika kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.


Mwenyekiti wa tawi la CCM DMV Loveness Mamuya akiwakaribisha rasmi wageni walikwa kwenye futari ya pamoja ilioandaliwa na tawi la CCM DMV, Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani.


Baadhi ya wanachama wa CCM Tawi la DMV wakipata picha ya pamoja baada ya futari walioiyanda


Wanachama wa CCM Tawi la DMV na baadhi ya wageni wawili kutoka Londan Uingereza

Wageni wawili majirani wapendanao kutoka jijini London pia walihudhuria katika futari hiyo ilioandaliwa na ilioandaliwa na tawi la CCM DMV Jana Ijumaa Aug 3, 2012 katika ukumbi wa Hillandale Park iliyopo Silver Spring, Maryland Nchini Marekani

Katibu wa CCM DMV Jacob Kinyemi, kushoto akipata picha ya pamoja na Halima baada ya kumkabidhi rasmi kadi ya uwanachama wa CCM, Jana Ijumaa na kuwa mwanachama rasmi wa CCM.

Thursday, June 28, 2012

LIONS CLUB YACHIMBISHA VISIMA SHULE ZA MSINGI MINAZI MIREFU NA AIRWING KIPAWA JIJINI DAR

Diwani wa Kata ya Kipawa Bonah Kaluwa, akifungua moja ya bomba la maji ya kisima walichokabidhiwa na wahisani hao katika Shule ya Msingi ya Airwing Kipawa. Diwani Kaluwa ndiye aliyefanikisha mpango wa upatikanaji wa visima hivyo kupitia Lions Club.
Gavana wa Lions Club Internation Tanzania na Uganda, Satish Sherma, akitoa hotuba fupi kabla ya kukabidhi visima hivyo.
Gavana wa Lions Club Internation Tanzania na Uganda, Satish Sherma, akimvalisha beji ya Lions Club, Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa wakati wa makabidhiano ya visima hivyo.
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa (wa pili kulia), akizungumza jambo na Gavana wa Lions Club Internation Tanzania na Uganda, Satish Sherma (kushoto) na Katibu Mkuu wa Lions Club, Mustafa Kundrat.
Wanafunzi wa Shule za Minazi Mirefu na Airwing wakipiga makofi wakati wa kukabidhiwa visima hivyo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya Msingi Minazi Mirefu, Daniel Mwamakula (kulia), akitoa neno la shukurani kwa wahisani hao na wageni waalikwa.
Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kulia), akimkabidhi fedha Bakari Ally ambaye alikuwa msimamizi wa ujenzi wa visima hivyo.

YANGA SPORTS YAFANYA MAZOEZI KUJIFUA KAGAME CUP

Kifaa kipya cha Yanga, kutoka Simba Kelvi Yondani, akipiga mpira wakati wa mazoezi ya timu hiyo kujifua kwa ajili ya kujiweka sawa na mashindano ya Kombe la Kagame, mashindano yatakayofanyika jijini Dar es Salaam.
Mshambuliaji mpya wa Yanga, Simon Msuva (mbele), akiwaongoza wenzake katika mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika kwenye fukwe za Coco Beach jijini Dar es Salaam jana. Wanaomfuatia ni beki mpya wa klabu hiyo, Kelvin Yondani na Godfrey Taita. (Picha zote na Mpiga Picha wa Habari Mseto Blog).
Nurdin Bakari akijifua wakati wa mazoezi hayo jana.
Nizar Khalfan (kushoto), akijifua na wachezaji wenzake wa Yanga katika mazoezi hayo.
Mmoja wa wachezaji wapya wa Yanga akiwa kwenye mazoezi hayo.

Wachezaji wa Yanga wakikimbia katika mazoezi mepesi ya kujiandaa na mashindano ya Kagame Cup yanayotarajiwa kuanza Julai 14 jijini Dar es Salaam.
Nizar Khalfan akiwa katika mazoezi na timu yake mpya ya Yanga katika ufukwe wa Coco Beach Oysterbay jijini Dar es salaam.
Wachezaji wa Yanga wakipiga danadana, wakati wa mazoezi yao kwenye ufukwe wa Coco Beach, jijini Dar es Salaam leo.

NYOTA WA NIGERIA OMOTOLA JALADE ATEMBELEA YATIMA JIJINI DAR

<><> <><> <><>
Mchezaji wa Filamu kutoka nchini Naigeria Omotola Jalade katikati akiwa katika picha ya pamoja na mwigizaji Wema Sepetu (kushoto) na Khadija Mwanamboka pamoja na watoto yatima wa kituo cha Tanzania Mitindo House cha jijini Dar es Salaam leo. Omotola amekuja nchini maalum kwa ajili ya uzinduzi wa filamu ya Wema Sepetu Super Star ambayo imezinduliwa jana kwenye hoteli ya Hyyat Kilimanjaro jijini Dar es salaam.


Omotola Jalade akiwasili kituoni hapo leo.

Omotola Jalade na Wema Sepetu wakiwa katika picha ya pamoja na watoto yatima wa kituo cha Tanzania Mitindo House.

MBUNGE ZUNGU (ILALA) AKUTANA NA WAKAZI WA SHARIF SHAMBA JIJINI DAR

Mkazi wa Sharifu Shamba, Abdallah Kondo, akitoa duku duku lake kwa Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan 'Zungu', wakati Mbunge huyo, alipofika eneo hilo kwa ajili ya kusikiliza matatizo ya wapiga kura wake na kuzungumza nao jijini leo. (Picha zote na Kassim Mbarouk)
Baadhi ya wakazi wa Sharif Shamba, wakisikiliza hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na baadhi yao kuhusu matatizo yanayowakabili kwenye eneo lao hilo, mbele ya Mbunge wao, Mussa Zungu, wakati alipowatembelea kusikiliza matatizo yao leo.
Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan 'Zungu', (wa pili kushoto), akiwa na Diwani wa Kata ya Ilala, Edson Fungo (wa tatu) na Mwenyekiti wa mtaa wa Sharif Shamba, Mtoro Shah, wakisikiliza hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na wakazi wa mtaa huo, wakati alipofika eneo hilo kwa ajili ya kusikiliza matatizo ya wapiga kura wake na kuzungumza nao jijini leo.
Mkazi wa Sharif Shamba, Ilala jijini Dar es Salaam, Mariam Mkupama, akitoa baadhi ya kero zinzowakabili mtaani hapo kwa Mbunge wao Mussa Zungu, alipokuwa akisikiliza matatizo yao yanayowakabili mtaani hapo leo.
Baadhi ya wakazi hao wakiwa katika mkutano huo leo, wakisikiliza masuala mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa na baadhi yao kwa Mbunge wao Mussa Azzan Zungu, alipofika mtaani hapo kusikiliza matatizo yao na kuzungumza nao.
Mbunge wa Ilala, Mussa Zungu (wa pili kushoto), akiwa na uongozi wa Kata ya Ilala na wa mtaa wa Sharif Shamba, akinakili matatizo na hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na kuwasilishwa kwake na wakazi wa Sharif Shamba, wakati alipokwenda kusikiliza matatizo yao pamoja na kuzungumza nao leo jioni.
Bi. Mtumwa Abdallah, akitoa matatizo yanayowakabili mtaani hapo mbele ya Mbune wa Ilala, Mussa Zungu (hayupo pichani), aliyotaja kuwa ni adha ya magari makubwa ambayo huuingizwa mtaani hapo na kusababisha kukata waya za umeme, hatua inayopelekea kuikosa nishati hiyo mara kwa mara.
Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan 'Zungu', (wa pili kushoto), akisoma moja ya barua aliyokabidhiwa na mmoja wa wakazi wa mtaa wa Sharif Shamba, kuhusiana na njia mbalimbali alizokuwa akipitia katika kutatua baadhi ya matatizo yao lakini bila kupata mafaniko yoyote yale. Wa tatu ni Diwani wa Kata ya Ilala, Edson Fungo, Mwenyekiti wa mtaa wa Sharif Shamba, Mtoro Shah (wa kwanza kushoto) na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa mtaa huo, Zadock Munisi, wakiwa katika mkutano huo.
Baadhi ya akinamama wakazi wa mtaa wa Sharif Shamba, wakisikiliza hoja mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa kwa Mbunge Zungu leo jioni.
Wananchi wakazi wa mtaa huo, wakimsikiliza Mbunge wao, Mussa Zungu alipokuwa akijibu hoja zao, walizokuwa wakizitoa kwake na kwa uongozi wa Kata na mtaa wao huo.
Mbunge wa Ilala, Mussa Zungu akizungumza na wakazi wa mtaa wa Sharif Shamba mara baada ya kusikiliza hoja na matatizo yao kwenye mkutano wao huo leo jioni.
Baadhi ya wakazi wa mtaa huo, wakimsikiliza Mbunge wao, Mussa Zungu, wakati alipokuwa akizungumza nao kwyenye mkutano huo leo jioni.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Sharif Shamba, Mtoro Shah, akijibu baadhi ya tuhuma alizokuwa ametuhumiwa na kuwasilishwa kwa mbunge Zungu (kulia), kwenye mkutao huo.
Mbunge wa Ilala, Mussa Zungu (katikati), Diwani wa Kata ya Ilala, Edson Fungo (kulia) na Mwenyekiti wa mtaa wa Sharif Shamba, Mtoro Shah (kushoto), wakisikiliza maelezo mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa kwa awamu ya pili na wakazi wa Sharif Shamba kwenye mkutano huo leo jioni.
Mkazi wa mtaa huo, Sakina Juma, akiwasilisha kwa Mbunge Zungu kilio chao, mtaani hapo, ikiwemo tatizo la maji na kuaharibika kwa pumpu ya kisima chao kirefu cha maji wanayotumia mtaani hapo, ambapo katika jibu lake Mbunge Zungu aliahidi kushughulikia tatizo hilo haraka ikiwemo kutoa tenki la kuhifadhia maji ya matumizi ya mtaa huo.
Mbunge Mussa Azzan Zungu, akizungumza na wakazi hao wakati alipokuwa akihitimisha mkutano wake na wakazi hao katika kusikiliza matatizo yanayowakabili pamoja na kero mbalimbali mtaani hapo. Wa pili kulia ni Diwani wa Kata ya Ilala, Edson Fungo, Mwnyekiti wa mtaa huo, Mtoro Shah (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM wa tawi la Sharif Shamba, Zadock Munisi